Mgomo wa Wafanyakazi
wa Uwanja wa Ndege wa Kenya Wasababisha Usumbufu wa Safari za Ndege kutokana na
Mpango wa Adani
Mgomo wa wafanyakazi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Jomo Kenyatta (JKIA) jijini Nairobi umesababisha ucheleweshaji mkubwa wa safari
za ndege na kughairishwa kwa baadhi ya safari, Kenya Airways ilitangaza
Jumatano. Hatua hii ya mgomo, inayoongozwa na Muungano wa Wafanyakazi wa
Usafiri wa Anga wa Kenya, inatokana na upinzani dhidi ya mpango unaopendekezwa
wa kuukodisha uwanja huo kwa Kampuni ya Adani kutoka India kwa muda wa miaka
30.
Muungano huo, unaowakilisha sehemu kubwa ya wafanyakazi wa
sekta ya usafiri wa anga nchini Kenya, ulionya kuwa mpango huo, ulitangazwa kwa
mara ya kwanza mwezi Julai, utasababisha kupotea kwa ajira na kuchukua nafasi
ya wafanyakazi wa Kenya na wageni kutoka nje.
Mgomo huo umeathiri safari za kuingia na kutoka uwanjani, na
kusababisha usumbufu kwa maelfu ya abiria. Kenya Airways iliwataka wasafiri
kufuatilia taarifa za safari za ndege na mabadiliko yoyote huku mazungumzo
yakiendelea kati ya muungano huo na serikali.
Mpango wa ukodishaji umekumbwa na utata, ambapo wakosoaji
wanasema kuwa unahatarisha ajira za ndani na mustakabali wa sekta ya usafiri wa
anga nchini Kenya.


0 comments: