WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameishukuru Serikali ya Denmark kwa misaada ambayo imekuwa ikiitoa kwenye miradi ya maendeleo nchini ambapo Krona milioni 1.95 (sh. bilioni 645.86) zilizotolewa katika kipindi cha miaka mitano.
Ametoa shukrani hizo leo (Jumatatu, Julai 15, 2024) wakati akizungumza na Balozi wa Denmark anayemaliza muda wake nchini, Bi. Mette N. Dissing-Spandet kwenye ofisi ndogo ya Magogoni, jijini Dar es Salaam.
0 comments: